IQNA

Maqari wa Kiirani wasoma Qur’ani Tukufu katika Mawkib jijini Karbala

QNA – Msafara wa Qur’ani wa Arbaeen kutoka Iran, unaojulikana mwaka huu kama “Msafara wa Imam Ridha (AS)”, ulianza shughuli zake katika njia ya Arbaeen tarehe 8 Agosti 2025.

 

Mmoja wa wanachama wa msafara huo wa Qur’ani alisoma Qur’ani Tukufu ndani ya Mawkib moja huko Karbala.

Mawkib ni vituo vya huduma vilivyo katika maeneo ya kidini ya Waislamu wa madhehebu ya Shia au wakati wa matukio ya kidini ya Mashia ambapo wafanyaziara na watu wengine wote katika eneo husika wanaweza kupokea chakula, chai, na sharbat (vinywaji vitamu) n.k na pia kupata sehemu ya kupumzika.

Wanachama wa ujumbe huu walifanya programu mbalimbali za Qur’ani kwa ajili ya wafanyaziyara wa Arbaeen wakati wa ukaaji wao nchini Iraq.

Mehdi Gholamnejad na Mehdi Taghipour, maqari wawili maarufu kutoka Iran, walikuwa katika msafara huo na wakasoma aya tukufu wakati wa matembezi ya kuelekea kwenye haram mbili tukufu mjini Karbala.

Ifuatayo ni qira’a yao ya Qur’an Tukufu ndani ya Mawkib ya  Atabat Muqaddasayn katika mji mtukufu wa Karbala:

4299990

Kishikizo: arbaeen ، qurani tukufu ، msafara ، iran
Habari zinazohusiana