IQNA

Mkutano wa Kimataifa wa Sanaa ya Kiislamu Pakistan

10:49 - November 12, 2008
Habari ID: 1707388
Mkutano wa kimataifa wa Sanaa na Usanifu Majengo wa Kiislamu unatazamiwa kuanza Alkhamisi ya wiki hii katika kitivo cha Sanaa mjini Lahore nchini Pakistan.
Wataalamu kutoka nchi za Iran, Canada, Bangladesh, India, Jordan, Lebanon, Uingereza, Umoja wa Falme za Kiarabu na Pakistan wamewasilisha makala mbalimbali katika mkutano huo.
Lengo la mkutano huo unaosimamiwa na Kitivo cha Sanaa cha Chuo cha Lahore, Chuo Kikuu cha Punjab na jumba la makumbusho la mji wa Lahore ni kustawisha utafiti katika nyanja za sanaa na usanifu majengo wa Kiislamu. 318868
captcha