Kwa mujibu wa Adel bin Ali as-Sha'ri, katibu mkuu wa Idara ya Kimataifa ya Kumfahamu Mtume (saw), maonyeshao hayo yameandaliwa na Idara ya Utamaduni na Uhubiri ya Sharjah, ambapo vitabu mbalimbali vinavyozungumzia maisha, tabia, sunna na kumfahamu Mtume (saw) na vilivyotarjumiwa kwa lugha mbalimbali vimeonyeshwa katika maonyesho hayo. Mashirika 491 ya vitabu yameshiriki katika maonyesho hayo, ambayo pia yameshuhudia kufanyika shughuli nyingine za fasihi na utamaduni. 319836