Mwezi Oktoba uliopita, gazeti hilo lilichapisha makala mbili ambazo zilitusi na kuwakosea heshima Waislamu. Vilevile moja ya vikatuni vilivyochapishwa na magazeti ya Denmark na kuzusha maandamano na malalamiko makubwa ya Waislamu ulimwenguni pia kilichapishwa katika gazeti hilo hivi karibuni. Gazeti hilo linalochapishwa nchini Russia ni sawa kabisa na lile linalochapishiwa nchini Marekani lakini likiwa na tofauti hii kwamba gazeti linalochpishiwa mjini Moscow linachapishwa kwa lugha ya Kirusi na makala zake nyingi zinahusiana na siasa za serikali ya Russia. Ni vyema kuashiria hapa kwamba, Russia ina Waislamu wapatao milioni ishirini. 322779