Warsha ya Sanaa ya Kiislamu katika Tamaduni tofauti imefanyika mjini Doha, Qatar kwa lengo ya kuchunguza utajiri wa sanaa ya Kiislamu. Warsha hiyo imefanyika sambamba na maonyesho ya kwanza ya muda ya Jumba la Makumbusho la Sanaa ya Kiislamu la Doha.