Kwa mujibu wa Mwambata wa Utamadauni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Istanbul Uturuki, maonyesho hayo yanafanyika kwa munasaba wa sikukuu ya Iddul Adha.
Mohammad Sadeqizadeh amesema, maonyesho hayo ya Asmaul Husna yanafanyika kwa ushirikiano wa Idara ya Utamdauni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Istanbul, Jumba la Makumbusho la Sanaa za Kisasa la Iran na Idara ya Utamaduni ya Baraza la Mji wa Istanbul.
Ameongeza kuwa maonyesho hayo yatakuwa na zaidi ya athari 70 na bora zaidi za wanakaligrafia Waiirani.
Sadeqizadeh amesema kuwa waandishi wa hati za Quran na Hadithi za Mtume SAW nchini Uturufki wanaheshimiwa sana kutokana na kuwa sanaa hiyo inahesabiwa kuwa kazi tukufu. 327442