IQNA

Madrasa ya Qur'ani yatia fora Kyrgyzstan

11:16 - December 03, 2008
Habari ID: 1715248
Madrasa moja ya Qur'ani huko nchini Kyrgyzstan katika kijiji cha “Alexandar Afka” iliyoandaa mafunzo ya sayansi za Qur'ani na maarifa ya Kiislamu imetambuliwa kama moja ya taasisi yenye harakati nyingi za Kiislamu katika mji mkuu wa nchi hiyo.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA nchini Kyrgyzstan, madrasa hiyo iitwayo “Darul Qur'ani” iliyo katika kitongoji cha mji mkuu wa Jamhuri ya Kyrgyzstan, Bishkent, imewavutia wanafunzi wengi kutokana na masomo yake ya hali ya juu.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, kuna zaidi ya wanafunzi 90 wanaosoma Qur'ani katika chuo hicho.
Mbali na kutoa mafunzo ya Qur'ani, waalimu katika chuo hicho wanafunza pia masomo mengine ya Kiislamu na wanasisitiza juu ya wanafunzi kuhudhuria masomo yote bila kufeli.
Masomo katika Madrassa ya Darul Quran kijijini Alexandar Afka hufanyika siku sita kwa wiki.
328535

captcha