IQNA

Tehran yakumbwa na majonzi katika Ibada ya kuaga mwili wa Imam Shahidi

IQNA – Ibada ya kuaga mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyed Ali Khamenei (Mwenyezi Mungu awe radhi naye), imeendelea kwa siku ya pili leo tarehe 5 Julai 2026, katika Ukumbi wa Sala wa Imam Khomeini (RA) uliopo Tehran. Mji wa Tehran umezama katika majonzi mazito huku mamilioni ya waombolezaji wakimiminika katika eneo la Musalla ili kutoa heshima za mwisho kwa shakhsia huyu mahiri na mlinzi wa Ummah. Hali ya huzuni imetawala kote, huku nyoyo za Waislamu zikiwa zimejaa msiba mkubwa wa kuondokewa na kiongozi wao shujaa aliyesimamia haki dhidi ya dhulma za ulimwengu.
 
 
Habari zinazohusiana