Viongozi wa ngazi za juu, wanasiasa mashuhuri, wasomi, na wawakilishi kutoka nchi mbalimbali wamewasili katika mji mkuu wa Iran ili kutoa heshima zao za mwisho na kumuaga Kiongozi huyo shahidi.
Katika hafla hiyo ya huzuni na utukufu wasomi wa Qur’an mashuhuri kutoka Iran, akiwemo Masoud Sayyah Gorji, Hamidreza Ahmadivafa, na Mehdi Adeli, walisoma aya tukufu za Qur’an, wakikumbusha juu ya fadhila za shahada na subira.
Mapema katika hafla hiyo, wanazuoni na viongozi wa kidini kutoka Indonesia, Afghanistan, Lebanon, Iraq, Morocco, Uturuki, na Uhispania walitoa heshima zao kwa mwili mtukufu wa Kiongozi shahidi. Vilevile, wawakilishi wa jumuiya za wachache wa kidini nchini Iran walijumuika kutoa heshima zao mbele ya familia ya marehemu na mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi.
Wajumbe kutoka harakati ya Kata’ib Hizbullah ya Iraq pamoja na kundi la viongozi waandamizi wa Mhimili wa Muqawama (Upinzani) walifuata kutoa heshima zao. Vilevile, makundi mengine yaliyoshiriki ni pamoja na wajumbe wa Mujahidina wa Jeshi la Kujitolea la Iraq (PMU), vuguvugu la Nujaba la Iraq, magavana wa miji ya Karbala na Najaf, na wawakilishi wengine wa Iraq.
Mhimili wa Muqawama uliwakilishwa kwa nguvu, huku wajumbe wa harakati ya Amal ya Lebanon na kundi la Mashia kutoka nchi za Ghuba ya Uajemi wakijumuika. Aidha, ujumbe wa ngazi ya juu wa Muqawama i wa Afghanistan, ukiongozwa na Ahmad Massoud, kiongozi wa Mhimili wa Kitaifa wa Muqawama wa Afghanistan, walikuwepo kuhuisha ahadi yao ya uaminifu.
Viongozi wa dini na wanazuoni kutoka mataifa mbalimbali, ikiwemo Mashia wanazuoni kutoka Pakistan, ujumbe wa Fatemiyoun kutoka Afghanistan, Baraza Kuu la Waislamu la Georgia, wabunge na viongozi wa Chama cha Revival cha Bulgaria, na wawakilishi wa vyama vya siasa na dini kutoka Uturuki walihudhuria. Pia walikuwepo wanazuoni Waislamu kutoka Russia, viongozi wa jamii ya Wahindu, kundi la Mashia kutoka Thailand na Ujerumani, pamoja na wawakilishi wa Popular Front for the Liberation of Palestine. Waandishi wa habari, waandishi wa vitabu, na wachambuzi kutoka Iraq, Lebanon, na Afghanistan nao hawakubaki nyuma katika kutoa buriani.
Heshima za pekee zilitolewa na ujumbe kutoka Hizbullah ya Lebanon, ikijumuisha familia ya Shahidi Syed Hassan Nasrallah, familia ya Shahidi Imad Mughniyeh, na familia za makamanda wengine mashahidi wa Hezbollah nchini Lebanon, wakitoa buriani kwa mwili mtukufu wa Kiongozi Shahidi.
Miongoni mwa wageni wengine wa kimataifa, wajumbe kutoka Malaysia, Lebanon, Russia, Senegal, Marekani, Mexico, Bosnia na Herzegovina, Hungary, China, Pakistan, Tunisia, India, Afghanistan, Norway, Argentina, na nchi kadhaa za Amerika ya Kusini wapo eneo la tukio. Pia, wasomi mashuhuri wa ulimwengu wa Kiislamu na wanaharakati wa umoja wa madhehebu ya Kiislamu kutoka nchi nyingi wameungana katika hafla hii.
Kwa mujibu wa msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, shughuli hii inahudhuriwa na wageni kutoka takribani nchi 100, wakiwemo wakuu wa nchi, maspika wa mabunge, mawaziri wa mambo ya nje, wawakilishi maalumu wa serikali, na viongozi wa kijamii na kidini.
Ikumbukwe kuwa, Ayatullah Seyed Ali Khamenei aliuawa shahada kufuatia shambulio la kigaidi lililofanywa na Marekani na utawala wa Kizayuni katika ofisi yake jijini Tehran mnamo Februari 28, 2026, mwanzoni mwa vita vya uchokozi vya siku 40 dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Mgogoro huo ulishuhudia operesheni kubwa za kulipiza kisasi na Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambazo ziliwalazimisha wachokozi kusitisha kampeni yao ya kijeshi.
3498066