IQNA

Kwa mara ya kwanza, shughuli ya kubadili pazia la al Kaaba yaonyeshwa katika televisheni ya Saudi Arabia

10:43 - December 08, 2008
Habari ID: 1717155
Shughuli ya kubadili pazia la Nyumba Tukufu ya Mwenyezi Mungu al Kaaba iliyofanyika jana sambamba na ibada ya kusimama kwenye uwanja wa Arafa imeonyeshwa moja kwa moja katika televisheni ya Saud Arabia na kituo cha intaneti cha Idara Kuu ya Masuala ya Masjidul Haram na Masjidun Nabii (saw).
Shirika rasmi la Habari la Saudi Arabia (SPA) limemnukuu Naibu Mwenyekiti wa Idara ya Masuala ya Masjidun Nabii Muhammad bin Nasir al Khaziim akisema kuwa shughuli hiyo ya kubadilisha pazia la al Kaaba ilihudhuriwa na wawakilishi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu na kwamba pazia hilo lilitengenezwa katika karakana ya kushona pazia la al Kaaba mjini Makka. Pazia hilo limeshonwa kwa kutumia kitambaa cha hariri na dhahabu halisi.
Muhammad bin Nasir amesema, juu ya mkanda uliaotumiwa kufunga pazia hilo la Nyumba ya Mwenyezi Mungu kumeandikwa aya za Qur'ani Tukufu. 331046


captcha