IQNA

Rais Ahmadinejad atoa mkono wa Idi kwa viongozi wa nchi za Kiislamu

10:32 - December 09, 2008
Habari ID: 1717401
Rais Mahmoud Ahmadinejad wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa salamu za pongezi kwa viongozi wote wa Kiislamu duniani kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Adh'ha .
Katika ujumbe wake huo, Rais Ahmadinejad ametoa salamu za pongezi, heri na fanaka kwa serikali na matiafa yote ya Waislamu kwa mnasaba wa sikukuu ya Idul Adh'ha.
Rais wa Iran ameitathmini sikukuu ya Idul Adh'ha kuwa dhihirisho la ibada kwa Mwenyezi Mungu.
Rais Ahmadinejad amemuomba Mwenyezi Mungu ayape mataifa yote ya Kiislamu mafanikio, heshima na furaha.
Aidha ametoa wito kwa Waislamu na nchi za Kiislamu kote duniani kudumisha umoja na mshikamano.
Wakati huo huo Rais Ahmadinejad amemtumia ujumbe Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu Prof. Ekmeleddin Ihsanoglu na kumpongeza kwa munasaba wa kuwadia sikukuu ya Idul Adh'ha. 331657
captcha