Hayo yamesemwa na Waziri wa Waqfu na Masuala ya Kidini wa Aljeria Bu Abdullah Ghulamullah ambaye ameongeza kuwa, si sahihi kwamba viongozi wa serikali ya Ufaransa ndio waliowasha moto katika msikiti huo.
Ghulamullah mesema: Makundi ya kisiasa yenye misimamo mikali na fikra za kibaguzi yanapinga suala la kuwepo uhusiano mzuri na maisha ya amani kati ya wafuasi wa dini na tamaduni tofauti na hayaheshimu haki za binadamu na za kiraia. Waziri wa Waqfu wa Aljeria amesisitiza kuwa, vitendo viovu vya makundi ya kibaguzi na yenye misimamo mikali ya Ufaransa dhidi ya vituo na taasisi za Kiislamu vinakwamisha mwenendo wa kuimarisha uhusiano mzuri na maisha ya amani kati ya wafuasi wa dini mbalimbali nchini Ufaransa. 337011