IQNA

Mashambulizi ya Israel huko Gaza yajadiliwa katika mkutano wa Umoja wa Kiislamu London

9:44 - December 30, 2008
Habari ID: 1724781
Washiriki katika mkutano wa Umoja wa Kiislamu mjini London, Uingereza wamejadili mashambulizi ya kinyama yanayoendelea kufanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Mkutano huo wa Umoja wa Kiislamu unahudhuriwa na maulamaa na wanafikra wa Kiislamu kutoka nchi mbalimbali.
Katika siku ya pili ya mkutano huo, hadhirina walijadili changamoto zinazoukabili umoja wa Kiislamu, mchango wa viongozi wa ngazi za juu wa kidini katika kufanikisha mshikamano wa Kiislamu na sisitizo la kuwepo mwamko wa Kiislamu. 340099
captcha