Gazeti la Jakarta Post limeandika kuwa, maelfu ya maulamaa na wanafunzi wa Kiislamu wa Ache Indonesia wamekusanyika katika msikiti mkuu wa jamaa wa mji huo wakiwaombea dua Wapalestina waliouawa shahidi katika mashambulizi ya kinyama ya utawala ghasibu wa Israel huko Gaza na kutangaza kuwa iwapo serikali itaruhusu, wako tayari kwenda kupigana jihadi huko Palestina.
Viongozi waliohutubia mkusanyiko huo wamelaani jinai za Israel katika Ukanda wa Gaza na kuashiria kuwa wanawake na watoto wadogo ndiyo wahanga halisi wa mashambulizi hayo. 345913