Wakizungumza na waandishi habari huko Cairo, madaktari hao wamesema kuwa wameazimia kuwaonyesha walimwengu matukio na janga halisi la kibinadamu lililotekelezwa na Wazayuni katika ukanda huo.
Muhammad as-Sharii, mmoja wa madaktari hao amesema kuwa, yale aliyoyashuhudia huko Gaza hayajawahi kushuhudiwa katika kipindi chote cha historia ya mwanadamu.
Huku akionyesha picha za kutisha za wahanga wa mashambulio hayo ya kinyama, Daktari huyo ambaye alikuwa mjini Khan Yunis tokea kuanza kwa mashambulio hayo, amesema kwamba mambo aliyoyashuhudia kuhusiana na janga hilo yalifanana na filamu za kutisha kuliko hali halisi ya mambo.
Rashid Imam, daktari mwingine aliyekwenda huko kuwasaidia wananchi wa Palestina, anasisitiza kwamba hakuna shaka yoyote kwamba, utawala haramu wa Israel ulitumia silaha zilizopigwa marufuku kimataifa katika mashambulio yake hayo dhidi ya watu wasio na hatia katika Ukanda wa Gaza. Madaktari hao wamesema kuwa Israel ilitumia katika hujuma yake hiyo ya kijinai silaha ambazo zilikuwa zikikata miili ya wahanga katika vipande vidogovidogo. Madaktari hao wana lengo la kushirikiana na Jumba la Makumbusho la Holocaust ya Wapalestina, ambalo ni jumba la maonyesho lisilo na ukweli wa dhahiri lakini linasimulia ukweli halisi wa mambo, kwa ajili ya kuwafahamisha walimwengu jinai zilizotekelezwa na utawala wa Israel dhidi ya watu wasio na hatia huko Gaza. 354362