Ijtimai hiyo inayofanyika kwa lengo la kuhuisha misingi ya Uislamu na kueneza amani, inahudhuriwa na Waislamu wasiopungua milioni mbili na zaidi ya elfu sita miongoni mwao wanatoka katika nchi 152.
Katika shughuli hiyo Waislamu hutekeleza kwa pamoja ibada ya swala, kusoma Qur'ani, kuhudhuria vikao vya mawaidha na hotuba za maulamaa wa Kiislamu kuhusu misingi ya Uislamu, amani, ikhlasi, udugu na kusameheana.
Mkusanyiko huo wa ijtimai ndio mkubwa zaidi wa Kiislamu baada ya marasimu ya ibada ya hija.
Ni vyema kukumbusha hapa kuwa karibu asilimia 87 ya jamii yenye watu milioni 150 ya Bangladesh ni Waislamu. 356689