IQNA

13:18 - February 02, 2009
Habari ID: 1739026

Uchunguzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na matunda yake nchini Tajikistan

Kikao cha kielemu cha uchunguzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na matunda yake kinatazamiwa kufanyika tarehe sita Februari katika mji wa Khujand nchini Tajikistan.

Kikao hicho ambacho kitahudhuriwa na washairi, wahakiki wa historia na wataalamu wa siasa wa Tajikistan, kitachunguza Mapinduzi ya Miislamu nchini Iran na matunda yake katika nyanja mbalimbali.
Malenga wanne wa mji wa Khujand pia watasoma mashairi kuhusu Mapinduzi ya Kiislamu katika kikao hicho.
Kitengo cha Utamaduni cha Iran nchini Tajikistan pia kimeahidi kutoa zawadi kwa watu watatu watakaochapisha makala bora magazeti kuhusu Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na wanafunzi bora 30 wa shule za mji mkuu wa Tajikistan Doshambe watakaoandika makala au kutunga mashairi bora zaidi kuhusu maudhui hiyo.
Ni vyema kuashiria hapa kuwa Iran imo katika sherehe za kuadhimisha miaka 30 ya Mapinduzi ya Kiislamu yaliyoongozwa na hayati Imam Khomeini. 357346
captcha