Kwa mujibu wa gazeti la Bahrain la Ar-Rayah, Rais Mary McAleese ameyasema hayo alipokitembelea kituo kilichotajwa na kujionea mwenyewe athari na nyaraka za pekee na za aina yake za Qur'ani zilizoandikwa kwa mkono zinazohifadhiwa katika kituo hicho. Amesema, nyaraka hizo zinathibitisha utukufu na thamani kubwa ya utamaduni na ustaarabu wa Kiislamu katika zama tofauti pamoja na umuhimu unaotolewa na watu wa Bahrain kwa urithi wa ustaarabu wa Kiislamu.
Abdul Latif Jassim Kano, muasisi wa kituo hicho alimfafanulia Rais wa Ireland masuala mbalimbali kuhusiana na jumba la mambo ya kale, maktaba, msikiti, sanaa za Kiislamu, nyaraka zilizoandikwa kwa mkono za Qur'ani na Kiislamu pamoja na ukumbi wa mikutano wa Muhammad bin Khalifa Aal Khalifa wa kituo hicho.
Amesema, lengo la kuanzishwa kituo hicho ni kuwafahamisha walimwengu urithi wenye thamani kubwa wa utamaduni na ustaarabu wa Kiislamu pamoja na kuhifadhi huko nyaraka za kale za Kiislamu zilioandikwa kwa mkono.
Mwishoni mwa matembezi ya Rais wa Ireland katika kituo hicho, Abdullatif Jassim Kano alimkabidhi vitabu na zawadi nyinginezo za ukumbusho wa safari yake katika kituo hicho. 358679