IQNA

Wawakilishi wa Congresi ya Marekani waliotembelea Gaza:

Uharibifu na masaibu yaliyowapata watu wa Gaza vinatisha

12:39 - February 21, 2009
Habari ID: 1746617
Wawakilishi wawili wa chama cha Democrats katika Congresi ya Marekani waliotembelea Ukanda wa Gaza wamesema kuwa mashaka makubwa yanayowapa raia wa eneo hilo na kiwango kikubwa cha uharibu wa mashambulizi ya kijeshi ya utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya eneo hilo kinatisha mno.
Baada ya kutembelea makazi yaliyoharibiwa na mashambulizi ya Israel na kuzungumza na waathirika wa unyama huo, Brian Baird amesisitiza kuwa kusikiliza maelezo ya mauaji ya watoto waliokuwa majumbani na shuleni, mauaji ya watu wote wa familia moja na vitendo vya Israel vya kuzuia misaada ya kibinadamu kwa majeruhi vinaumiza mno moyo wa mwanadamu. Amesema, yaliyotukia Gaza na hali inayoendelea kulikumba eneo hilo inatikisa nyoyo na haiwezi kuelezeka kwa maneno.
Brian Baird na Keith Ellison ni wawakilishi wa kwanza wa Bunge la Marekani kutembelea eneo la Ukanda wa Gaza tangu harakati ya Hamas ichukue madaraka katika eneo hilo zaidi ya miaka miwili iliyopita.
Ellison ambaye ni mwakilishi wa kwanza na pekee Muislamu katika Bunge la Marekani amesema maelezo kuhusu maafa yaliyowapata watoto wadogo wa Gaza yanasikitisha sana. Amekosoa vikali hatua ya Israel ya kuzuia misaada ya kibinadamu kwa raia wa Gaza na akasisitiza kuwa malori yaliyosheheni misaada ya kibinadamu yamezuiwa kuingia Gaza wakati raia wa eneo hilo hususan wanawake na watoto wadogo, wakihitajia mno chakula, maji na tiba. 366730
captcha