Mkutano huo utajadili masuala mbalimbali ikiwa ni pamoja na mchango wa mivutano ya makundi mbalimbali katika kudhoofisha umma wa Kiislamu, njia za kulinda umoja na mshikamano wa Kiislamu na chuki na kidini.
Mkutano wa 12 wa kimataifa wa kukurubisha pamoja madhehebu za Kiislamu ulifanyika mwaka 2002 na ulichunguza sababu za kihistoria za hitilafu kati ya madhehebu za Kiislamu hususan kati ya Shia na Suni.
Mkutano huo ulisisitiza juu ya udharura wa kufanyika juhudi za kuepusha hitilafu kati ya makundi ya Kiislamu na kuwasaidia wananchi wanaodhulumika wa Palestina katika mapambano yao dhidi ya hujuma za Israel. 370233