IQNA

Mjumbe wa Marekani kukutana na viongozi wa kidini wa Lebanon

16:45 - March 09, 2009
Habari ID: 1753909
Mjumbe wa Ikulu ya Marekani White House katika eneo la Mashariki ya Kati amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa makundi ya kisiasa na kidini nchini Lebanon.
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Jeffrey Feltman amewasili Beirut baada ya kutembelea Damascus na kukutana na viongozi wa Syria.
Mjumbe wa Marekani Mashariki ya Kati alitazamiwa kukutana pia na Sheikh Abdulamir Qublan, Naibu Mwenyekiti wa Baraza Kuu la Waislamu wa Kishia, Mufti wa Lebanon Sheikh Muhammad Rashid Qabbani, kiongozi wa Wamaroni Samir Nasrullah Safir na Mkuu wa kundi la Lebanese Forces Samir Jaajaa. 374806

captcha