Hayo yamesemwa na Hujjatul Islam Walmuslimin Muhammad Ridha Nurullahiyan, Mshauri wa ofisi ya Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran ambaye ameongeza kuwa mataifa na umma wa Kiislamu unafuata fikra na itikadi za maulamaa kuhusu suala la umoja wa Kiislamu.
Sheikh Nurullahiyan amesema kuwa Waislamu waliowengi wanafuata maulamaa na wasomi wanaoijua dini vizuri ambao daima husisitiza juu ya udharura wa umoja na mshikamano wa Kiislamu.
Amekosoa misimamo ya makundi yenye misimamo mikali kama Mawahabi na akasisitiza juu ya umuhimu wa kukabiliana nayo.
Amesema kuwa maulamaa wa Kiislamu hawapaswi kunyamaza kimya mbele ya makundi kama hayo kwa sababu Uislamu unapata madhara makubwa kutoka na harakati zao. 378746