IQNA

Kongamano la Taswira ya Waarabu na Waislamu katika Fasihi ya Dunia kufanyika Damascus

15:15 - April 04, 2009
Habari ID: 1760074
Kongamano la “Taswira ya Waarabu na Waislamu katika Fasihi ya Dunia” litaanza kesho katika Chuo Kikuu cha Damascus nchini Syria.
Lengo la kongamano hilo limetajwa kuwa ni kupata marifa kamili kuhusu taswira ya Waarabu na Waislamu katika fasihi mbalimbali duniani na kuweka wazi sababu zinazopelekea kuchafuliwa sura ya Waislamu na Waarabu.
Washiriki katika kongamano hilo watachunguza maudhui ya taswira ya Waarabu na Waislamu katika nchi za Magharibi, Ulaya, Asia, Afrika na America ya Latini na taathira za itikadi za mashariki katika taswira hiyo.
382460
captcha