IQNA

Mashindano ya kitaifa ya Hadithi za Mtume nchini Qatar

12:14 - April 09, 2009
Habari ID: 1762317
Duru ya nne ya mashindano ya kitaifa ya kuhifadhi hadithi za Mtume Mtukufu (saw) yatakayofanyika chini ya anwani ya Khalid bin Abdullah bin Khalid Aal Thani yamepangwa kufanyika nchini Qatar siku ya Jumamosi.
Kwa mujibu wa gazeti la As-Sharq, mashindano hayo yatawajumuisha wanawake na wanaume katika makundi mbalimbali ya kiumri.
Salim al-Bakri, msimamizi mkuu wa mashindano hayo amesema kuhusiana na suala hilo kwamba, hadithi zitakazohifadhiwa kwa ajili ya mashindano hayo zimetolewa katika kitabu cha Umdatul Ahkam fi Kalami Kheiril Anam ambacho kimeandikwa na Abdul Ghani al-Maqdisi, mwandishi mashuri wa Kiislamu. Amesema hadithi hizo zimekusanywa katika kijitabu kidogo na kupewa walio na nia ya kushiriki katika mashindano hayo ili kujitayarisha. Kijitabi hicho pia kimesambazwa katika mashule na vituo vya kuhifadhi Qur'ani vinavyosimamiwa na Wizara ya Wakfu ya Qatar.
Al-Bakri amesema kuwa mashindano hayo yataendeshwa na timu ya marefa wenye uzoefu mkubwa kutoka Qatar. Zawadi nono zitatolewa kwa washindi wa mashindano hayo. 384854
captcha