Kwa mujibu wa gazeti la mtandano la nchi hiyo la al-Iqtisadiya, sherehe hizo zimesimamiwa na Amir Naif bin Abdul Aziz, Waziri wa Mambo ya Ndani wa Saudi Arabia na makamu wake Amir Muhammad bin Naif bin Abdul Aziz. Aidh al-Qarani, Mkuu wa Idara ya Mwongozo na Uhubiri wa Kiislamu ya nchi hiyo amesema kuwa lengo la kufanyika mashindano hayo lilikuwa ni kushajiisha na kuwahamasisha askari usalama na polisi ya nchi hiyo kuhifadhi Qur'ani Tukufu pamoja na kutekeleza mafundisho yake na kuleta mfungamano baina ya mafundisho na vitendo.
al-Qarani amesema kuwa watu 350 walishiriki katika mashindano hayo, ambapo 65 kati yao walifanikiwa kufikia hatua ya mwisho ya mashindano hayo. Amesema washindi 15 kati ya hao watapewa zaidi nono ya riali laki moja na nusu za Saudia.
Mashindano hayo yamefanyika katika hatua tano ambazo ni kuhifadhi juzuu 15, juzuu 10, juzuu 5, juzuu 3 na hatimaye juzuu moja ya kitabu kitakatifu cha Qur'ani. 390821