IQNA

Haki za binadamu zinafanywa wenzo wa madola makubwa kuidhibiti dunia

13:54 - April 28, 2009
Habari ID: 1771119
Msemaji wa Baraza la Kulinda Katiba ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa suala la haki za binadamu limefanywa wenzo wa kisiasa wa madola makubwa kwa ajili ya kudhibiti dunia.
Abbas Ali Kadkhudai ameyasema hayo katika kongamano la "Haki za Binadamu, Kuanzia Nadharia hadi Matendo" mjini Tehran na kuongeza kuwa wataalamu na wanasiasa kote duniani wameliweka suala la haki za binadamu katika siasa zao kuu. Amesema kuwa katika miongo miwili ya hivi karibuni wasomi na wanasiasa duniani wamelipa umuhimu mkubwa suala la haki za binadamu kutokana na umuhimu wake.
Kadkhudai amesema kuwa suala hilo limekuwa wenzo wa kisiasa unaotumiwa na madola makubwa kwa ajili ya kuidhibiti dunia.
Msemaji wa Baraza la Kulinda katiba amesisitiza kwamba kuna udharura wa kutambulika vyema haki za binadamu na kujadiliwa katika duru za kielimu. 395516


captcha