Mkutano huo unaosimamiwa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Morocco unahudhuriwa na wasomi, watafiti na wahakiki kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu na Marekani.
Ajenda kuu ya mkutano huo ni kuchunguza historia ya utafiti na maandiko ya wataalamu wa masuala ya Mashariki (orientalist) wa Marekani kuhusu sira ya Mtume Muhammad (saw) na mbinu zao katika utafiti huo.
Maudhui nyingine zinazojadiliwa ni taswira ya Mtume Mtukufu katika mijadala ya kidini, fasihi, mbinu mbalimbali za masomo, vyombo vya habari na tafiti za wasomi na wataalamu wa Marekani wa masuala ya nchi za Mashariki. 399962