Mkutano huo umepangwa kufanyika Jumatano ijayo mjini Cairo Misri kujadili ugonjwa na homa ya mafua ya nguruwe nchini Saudi Arabia.
Mawaziri hao wanajadili njia za kuzuia maambukizi ya homa ya mafua ya nguruwe kwa mahujaji, kasi ya maambukizi ya ugonjwa huo duniani hususan katika eneo la Mashariki ya Kati na njia za kukabiliana na maambukizi yake.
Shirika la Afya Duniani WHO limetangaza kuwa Saudi Arabia imeahidi kwamba itachukua hatua za dharura za kuzuia maambikizi ya homa ya mafua ya nguruwe miongoni mwa mahujaji wa nyumba tukufu ya Mwenyezi Mungu na kusisitiza kwamba mahujaji hao wanapaswa kupata chanjo ya ugonjwa huo wiki mbili kabla ya kuelekea Makka kwa ajili ya ibada hiyo. :435594