IQNA

Msikiti mtukufu wa Makka watayarishwa kwa ajili ya mwezi wa Ramadhani

11:21 - August 07, 2010
Habari ID: 1968225
Uongozi wa masuala ya msikiti mtukufu wa Makka, Masjidul Haram na msikiti wa Mtume mjini Madina umetangaza kwamba maeneo hayo matakatifu yanatayarishwa kwa ajili ya mwezi wa Ramadhani.
Uongozi huo umesema kazi za kukarabati maeneo hayo matakatifu ikiwa ni pamoja na kutengeneza na kuweka viyoyozi vipya kwa ajili ya kuboresha hali kwa watu wataokazuru maeneo hayo matakatifu katika mwezi wa Ramadhani imekwishaanza.
Vilevile kumewekwa taratibu mpya za usafiri ili kusahilisha mambo kwa mahujaji na watu wanaozuru maeneo matukufu ya Makka na Madina katika mwezi wa Ramadhani.
Mwezi mtukufu wa Ramadhani unatazamiwa kuanza katikati ya wiki ijayo katika maeno mengi duniani. 627837

captcha