IQNA

Kongamano la "Uwekezaji wa Kiislamu na Uchumi wa Kisasa" kufanyika Qatar

14:15 - September 04, 2010
Habari ID: 1987027
Kongamano la 'Uwekezaji wa Kiislamu na Uchumi' wa Kisasa litafanyika baadaye mwezi wa Septemba katika mji mkuu wa Qatar Doha.
Kwa mujibu wa gazeti la As Sharq, kongamano hilo limeandaliwa kwa himaya ya Kituo cha Ushauri wa Kifedha cha Qatar. Bw. Ghanim bin Saeed Ale Saeed Mkuu wa Baraza la Kiidara la Kituo cha Ushauri wa Kifedha cha Qatar amesema kongamano hilo litahudhuriwa na mawaziri wa fedha, wakuu wa taasisi za utafiti wa kifedha na uchumi wa Kiislamu na wakuu wa benki kuu na taasisi za kifedha za nchi za Kiislamu. Ameongeza kuwa kongamano hilo litachunguza uwekezaji wa Kiislamu na masuala ya kiuchumi duniani.
647114
captcha