IQNA

Kuwasaidia Waislamu wa Pakistan ni kutekeleza mafunzo ya Qur'ani

14:29 - September 06, 2010
Habari ID: 1988587
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC ametoa wito kwa Waislamu duniani kote kutekeleza mafundisho ya Qur'ani kivitendo kwa kuwasaidia waliokumbwa na maafa ya mafuriko nchini Pakistan.
Ekmeleddin Ihsanoglu amesema kwa kufahamu ipasavyo mafundisho ya Qur'ani Tukufu tunaweza kuelewa vyema jinsi kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu kinavyoongoza katika masuala ya kuheshimu haki za binadamu.
Ihsanoglu amesema Qur'ani Tukufu daima inasisitiza juu ya suala la kutoa misaada ya kibinadamu na kuwasaidia wanaohitajia na wasiojiweza katika jamii. 649098
captcha