IQNA

Kongamano la kaligrafia ya Kiislamu lafanyika mjini Islamabad Pakistan

12:49 - September 23, 2010
Habari ID: 1999877
Kongamano la kaligrafia ya Kiislamu lilifanyika siku ya Jumanne Septemba 21 katika Nyumba ya Sanaa ya Taifa mjini Islamabad Pakistan.
Kwa mujibu wa gazeti la Daily Times, Muhammad Ilahi Bukhsh Muta, mwanakaligrafia mashuhuri wa Pakistan ndiye aliyesimamia kongamano hilo. Katika kongamano hilo Muta amewafundisha washiriki mbinu na njia za kufahamu kaligrafia ya Kiislamu na Qur'ani pamoja na kuwabainishia umuhimu wa sanaa hiyo katika nchi za Kiislamu na katika mashindano ya kimataifa. 660627
captcha