Kanisa la First United Methodist katika jimbo la Illinois nchini Marekani limeanza kutoa mafunzo ya Qur'ani Tukufu ikiwa ni katika juhudi za kusaidia kufahamika vyema kitabu hiki kitakatifu miongoni mwa Wamarekani, kufuatia wito wa kasisi mmoja mwenye chuki dhidi ya Uislamu wa kuchomwa moto kitabu hicho tarehe 11 Septemba.
Mafunzo hayo yanayotolewa chini ya anwani ya 'Usichome Qur'ani, Isome na Kuifahamu', yanawahimiza wakazi wa jimbo hilo kusoma tarjumi ya Kiingereza ya kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu na kuchunguza kwa makini maana ya maneno yake.
Malengo mengine ya masomo hayo ni kusaidia kueleweka vyema mafundisho na misingi ya Uislamu, kuwakurubisha pamoja wafuasi wa dini tofauti za mbinguni na kuimarisha maelewano katika jamii. 668649