IQNA

Wawakilishi wa vyombo vya habari kutoka nchi 50 washiriki katika maonyesho ya magazeti na mashirika ya habari mjini Tehran

13:59 - October 26, 2010
Habari ID: 2020171
Wawakilishi na wamiliki wa vyombo vya habari kutoka nchi 50 za dunia wanashiriki katika maonyesho ya 17 ya kimataifa ya magazeti na mashirika ya habari ambayo yalianza mjini Tehran hapo jana Jumatatu tarehe 25 Oktoba.
Nchi za Kenya, Iraq, Tajikistan, Uturuki, Argentina, China, Syria, Ufaransa, Palestina zilishiriki katika siku ya kwanza ya ufunguzi wa maonyesho hayo. Nchi nyingine za Tanzania, Uingereza, Albania, Belarus, India, Croatia, Misri, Lebanon, Korea Kusini, Yemen, Qatar, Libya, Georgia, Kuwait, Kyrgyzstan na Russia zinatazamiwa kushirikia katika maonyesho hayo tokea leo Jumanne.
Maonyesho ya 17 ya kimataifa ya magazeti na mashirika ya habari ya mjini Tehran yataendelea hadi siku ya Jumatatu tarehe Mosi Novemba. 682704
captcha