Mkuu wa masuala ya afya katika mji wa Makka Khalid Bin Abid Zafr amesema suhula za hospitali na kliniki katika miji ya Makka na Madina zitaimarishwa katika msimu wa Hija.
Afisa huyo ameongeza kuwa huduma za afya kwa mahujaji zitajumuisha matibabu ya dharura, kuzuia magonjwa, chanjo n.k. Amesema kuwa Shirika la Afya Duniani linashirikiana na maafisa wa afya wa Saudia katika kuzuia magonjwa ya kuambukizwa.
683234