Kikao hicho kitakachofanyika chini ya anwani ya 'Ubadilishwaji wa Jamii, Ujenzi wa Mustakbali wa Pamoja wa Waislamu na Wakristo', kitajadili wasiwasi huo na kuutafutia ufumbuzi wa pamoja ili kuimarisha shughuli za Kiislamu na Kikristo katika pembe mbalimbali za dunia.
Watakaohutubia kikao hicho ni pamoja na Qadhi bin Muhammad bin Talal, mwakilishi maalumu wa Mfalme Abdallah II wa Jordan, Kasisi Andres Wajrid kutoka Kanisa la Sweden na Ayatullah Muhammad Ali Taskhiri, Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kimtaifa ya Kukurubisha Pamoja Madhehebu ya Kiislamu kutoka Iran.
Washiriki wa kikao hicho watatembelea misikiti na makanisa mashuhuri ya Geneva na pia kukutana na viongozi wa jumuiya za kidini katika mji huo. Kwa Ujumla wazungumzaji 60 wamepangiwa kuhutubia kikao hicho. 683918