Hayo yamesemwa na Assane Samb, mhariri msaidizi wa gazeti la Lematindafrique na mwakilishi wa Senegal katika Maonyesho ya Kimataifa ya Magazeti na Vyombo vya Habari mjini Tehran.
Assane Samb amesema kuwa licha ya njama kubwa zilizofanywa na maadui wa Uislamu lakini hawajafanikiwa kusimamisha kasi ya dini hiyo katika nchi za Magharibi.
Ameongeza kuwa matukio ya kuchomwa Qur'ani nchini Marekani ni sehemu ya siasa za kupiga vita ustaarabu wa Kiislamu. Amesema kuwa woga wa Wamagharibi kuhusu kasi ya dini ya Kiislamu umewafanya hata viongozi wa Kikristo kama Terry Jones kuanzisha vita dhidi ya Uislamu na kwamba njama kama hizo haziwezi kufanikiwa.
Mhariri msaidizi wa gazeti la Lematindafrique amesema kuwa propaganda chafu dhidi ya Uislamu katika nchi za Magharibi hazilengi dini ya Kiislamu pekee bali utamaduni mzima wa wafuasi wa dini hiyo, tamaduni za Kiyahudi na wa Kikristo. 684889