IQNA

13:35 - November 09, 2010
Habari ID: 2028707

Kuenea fikra za Kiwahabi kunatia wasiwasi nchini Ufaransa

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Kiutamaduni na Kiislamu ya al Nur katika mji wa Dransy nchini Ufaransa Hassan Chalghumi ameelezea wasiwasi wake kutokana na kuenea fikra potofu za Kiwahabi nchini humo.

Hassan Chalghumi ambaye alikuwa akihutubia katika kituo cha Mayahudi mjini Lyon ameeleza wasiwasi wake mkubwa juu ya ongezeko la makundi yenye misimamo mikali ya Kiwahabi nchini Ufaransa na akasema kuwa kunawatia wasiwasi Waislamu wote wa Ufaransa.
Hata hivyo amesema kuwa Uislamu unaendelea kustawi nchini Ufaransa licha ya propaganda chafu zinazofanywa dhidi ya dini hiyo tukufu.
Amesema njia pekee ya kukabiliana na fikra za Kiwahabi na makundi potofu ni kuteuwa maimamu wa misikiti kutoka ndani ya Ufaransa kwenyewe ni si kuchukua maimamu hao kutoka nje ya nchi. 691768
captcha