IQNA

Awamu ya kwanza ya treni ya maeneo matakatifu kufungliwa leo Makka

15:56 - November 13, 2010
Habari ID: 2031112
Awamu ya kwanza ya treni itakayokuwa ikibeba mahujaji katika maeneo matakatifu ya Makka inafunguliwa rasmi hii leo.
Treni hiyo itatoa huduma kwa mahujaji na kusafirisha watu katika maeneo ya Mina, Arafat na Muzdalifa.
Treni hiyo itakuwa na uwezo wa kusafirisha mahujaji laki moja kwa saa baada ya kukamilika.
Treni hiyo itakamilika mwaka ujao na itakuwa na taathira kubwa katika kupunguza msongamano wa magari yanayosafirisha mahujaji katika maeneo matukufu ya Makka.
Awamu ya pili ya treni hiyo itaunganisha maeneo matakatifu na msikiti wa Makka. 694208

captcha