IQNA

Mwakilishi wa mamarja' Kuwait atuma salamu za pongezi kwa mnasaba wa kuzaliwa Masih (as)

12:35 - December 25, 2010
Habari ID: 2052651
Sayyid Muhammad Baqir al-Muhri, mwakilishi wa viongozi wakuu wa dini wa madhehebu ya Shia nchini Kuwait ametoa taarifa akiwapongeza walimwengu wote kwa mnasaba wa kuadhimishwa siku ya kuzaliwa Nabii Isa (as) na mwaka mpya wa Miladia wa 2011.
Taarifa hiyo imesema kuwa jina la Nabii Masih pamoja na la mama yake mtakatifu Maryam (as) yametajwa mara kadhaa katika Qur'ani Tukufu na kuwapongeza Waislamu na Wakristo kwa mnasaba wa kuzaliwa Nabii huyo Mtakatifu.
Sayyid al-Muhri ameelezea matumaini yake kwamba mwaka mpya ujao utakuwa mwaka wa heri, baraka, utulivu na usalama kwa walimwengu wote. Vilevile ameelezea metarajio kuwa ulimwengu hautashuhudia tena vitendo vya ugadi, vita na matatizo ya kijamii.
Al-Muhri ambaye pia ni Mkuu wa Baraza la Uhusiano wa Kiislamu na Ukristo la Kuwait ameendelea kusema kuwa Uislamu ni dini ya urafiki wa dhati, upondo, usamehevu na maisha ya amani ya pamoja na watu wengine na kwamba Waislamu pia husherehekea siku ya kuzaliwa Nabii Isa (as). Amesema ni makundi ya kitaasubi na yenye fikra potofu yanayowakufurisha watu pamoja na viongozi wao waovu tu ndio huwa na huzuni katika siku hii muhimu.
Sayyid Muhammad Baqir al-Muhri amesisitiza kwamba fiqhi ya Ahlul Bait (as) inajuzisha Waislamu kuwapongeza Wakristo kwa mnasaba wa kuzaliwa Nabii Isa (as) na kwamba mafundisho ya Kishia pia yanakataza wafuasi wake kuwafanyia khiana na maudhi majirani wasiokuwa Waislamu. 717385
captcha