Onyo hilo la Putin linafuatia matukio ya kusikitisha yaliyotokea katikati mwa nchi hiyo katika kipindi cha wiki chache zilizopita ambapo watu kadhaa walifanya vitendo vya kukosea heshima kitabu hicho kitakatifu. Putin amesisistiza juu ya umuhimu wa kuishi pamoja kwa amani watu wa Russia ambao wanafungamana na makundi tofauti ya imani na utamaduni.
Ameashiria hatari ya kuongezeka mielekeo ya utaifa na ubaguzi wa rangi nchini humo na kusema kuwa jamii mbalimbali za nchi hiyo zinapasa kushajiishwa suala la kuishi pamoja kwa amani na sio kuchochewa kujihusisha na vitendo vya ubaguzi wa kimbari na dini. 719038