Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA mjini Lusaka, Caleb Fundanga Gavana wa Benki Kuu ya Zambia amesema wafanyakazi wa benki hiyo wamepata mafunzo maalumu kuhusu mfumo wa benki za Kiislamu.
Fundanga amesema kuwa anasubiri sekta binafsi nchini humo itoe ombi la kuanzisha benki za Kiislamu nchini Zambia. Gavana wa Benki Kuu ya Zambia amesema benki hiyo iko tayari kupokea maombi ya kuanzishwa benki za Kiislamu nchini humo.
Fundanga ameelezea matumaini kuwa kuanzishwa benki za Kiislamu zinazotoa mikopo bila kutoza riba kwa wateja ni jambo ambalo litapugunza gharama za mikopo nchini humo.
721516