IQNA

Timu ya madaktari yashangazwa na athari mbaya ya silaha zilizopigwa marufuku huko Gaza

13:12 - January 10, 2011
Habari ID: 2061947
Timu ya madaktari wa Lebanon imeshangazwa na idadi kubwa ya watoto wa Ukanda wa Gaza waliolemazwa na silaha zilizopigwa marufuku zilizotumiwa na utawala haramu wa Israe katika mashambulio yake ya kinyama ya siku 22 katika eneo hilo.
Kwa mujibu wa tovuti ya Palestina Info, madaktari hao ambao walikuwa wakizungumza na waandishi habari baada ya kuyatembelea maeneo ya mashambulio hayo ili kutathmini hali ya afya ya eneo hilo wamesema kuwa Gaza imejaa watoto waliolemazwa na silaha hizo zilizopigwa marufuku zikiwemo za fosfori, urani uliyohafifishwa, mabomu ya vishada na silaha nyingine nyingi za kemikali.
Madaktari hao pia wametaka kuondolewa mara moja kwa mzingiro unaotekelezwa na utawala ghasibu wa Israel dhidi ya Ukanda wa Gaza ili kuwezeshwa kufikishwa misaada ya dharura kwa watoto na watu wengine wanaohitajia misaada ya kibinadamu na hasa ya kiafya na kitiba katika ukanda huo.
Askari wa Israel wanazuia kuingizwa katika ukanda huo shehena za kitiba na pia kuondoka wagonjwa wa ukanda huo ili kutibiwa katika nchi nyingine. Kutokana na mzingiro huo wagonjwa wengi wa ukanda huo wamekuwa wakipoteza maisha yao. 727189
captcha