Kwa mujibu wa tovuti ya chuo hicho Mtontana.edu, John L. Esposito, profesa wa masuala ya Kiislamu na kimataifa wa mjini New York anatazamiwa kuzungumza katika kikao hicho ambacho kitaanza saa moja usiku kwa wakati wa jimbo hilo. Mwanafikra huyo wa Kiislamu atazungumzia fikra potofu na tuhuma zinazotolewa na Wamagharibi dhidi ya Uislamu na Waislamu.
Esposito ni muhadhiri wa masuala ya Kiislamu na kimataifa katika Chuo Kikuu cha Georgetown. Kufikia sasa ameandika vitabu na makala 35 yanayohusiana na Uislamu na kitabu chake cha hivi karibuni ni kile kinachohusiana na mustakbali wa Uislamu kilichochapishwa mwaka uliopita wa 2010. 740257