Jumuiya ya Waislamu Ghana ikishirikiana na Idara ya Utamaduni ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Accra imeanzisha gazeti hilo la kwanza la Waislamu katika nchi hiyo ya Afrika Magharibi. Toleo jipya la jarida hilo lina maudhui kama vile ‘Maadili kwa Mtazamo wa Imam Khomeini’ na vile vile matukio muhimu ya Mapinduzi ya Kiislamu.
Waislamu nchini Ghana wamekaribisha gazeti hilo ambalo wanasema litakuwa la kwanza na la aina yake kuakisi hali na mitazamo ya Waislamu nchini humo.
749030