IQNA

Warsha ya “Maumbile Asilia kwa Mtazamo wa Sayansi na Qur'ani”

15:22 - February 27, 2011
Habari ID: 2086790
Warsha yenye anwani ya “Maumbile Asilia kwa Mtazamo wa Sayansi na Qur'ani” imefanyika Februari 26 huko Jordan.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Dastur warsha hiyo ni kati ya mfululizo wa vikao kuhusu muujiza wa kisayansi katika Qur'ani Tukufu. Vikao hivyo vimeandaliwa na Jumuiya ya Muujiza wa Kisayansi na Qur'ani na Sunna nchini Jordan. Warsha hiyo iliandaliwa na Jumuiya ya Fasihi ya Kiislamu ya Jordan.
Ali Al Mar mtaalamu wa mujiza wa Qur'ani ametoa hotuba katika warsha hiyo. Warsha hiyo imehudhuriwa na wataalamu pamoja na watu wa kawaida wanaovutiwa na mada hiyo.
753626

captcha