IQNA

Salamu za rambirambi za Katibu Mkuu wa OIC kwa watu wa Japan

13:58 - March 14, 2011
Habari ID: 2095482
EkmeleddinIhsanoglu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC ametuma salamu za rambirambi kwa serikali na taifa la Japan kufuatia mtetemeko mkubwa wa ardhi uliotokea hivi karibuni nchini humo na kusababisha maafa na hasara kubwa.
Kwa mujibu wa tovuti ya OIC Ihsanoglu amesema kuwa Waislamu katika ulimwengu wa Kiislamu wana wasiwasi mkubwa kuhusiana na maafa yaliyowapata wanadamu wenzao huko Japan na kuongeza kuwa jumuiya ya OIC pamoja na nchi zote wanachama ziko tayari kuwasaidia wananchi wa nchi hiyo kwa msaaada wowote ule wanaoweza kutoa.
Amesema anatumai hali ya nchi hiyo itarejea katika hali ya kawaida hivi karibuni. 763247
captcha