Sheikh Salman amepinga kila aina ya uingiliaji wa mambo ya ndani ya nchi hiyo kutoka upande wowote ule. Amesema licha ya kuwa Bahrain ina hamu kubwa ya kuimarisha uhusiano wake na kila nchi jirani lakini haiko tayari kukubali uingiliaji wa nchi hizo katika mambo yake ya ndani. Baada ya kuthibitishwa ripoti za kuingia askari jeshi wa Saudi Arabia nchini Bahrain kwa lengo la kuzima mapambano ya wananchi dhidi ya wafalme dhalimu wa nchi hiyo, maadui wa Iran wameeneza uvumi kwamba jumuiya za Kishia za Bahrain kutoka Iran zimekuwa zikiingia nchini humo kuwasaidia ndugu zao wanaokandamizwa na askari wa nchi hiyo kwa ushirikiano wa askari wa Saudia. 764186