IQNA

Hasira ya Wasaudia kuhusiana na kukosewa heshima Qur'ani Tukufu nchini humo

11:38 - March 31, 2011
Habari ID: 2099288
Kitendo cha kutupwa nuskha 200 za Qur'ani Tukufu kwenye kituo cha kufukia taka huko katika mkoa wa Taif nchini Saudi Arabia kimewakasirisha sana wananchi wa nchi hiyo.
Nuskha hizo za Qur'ani zilipatikana zikiwa zimetupwa kwenye taka hizo hapo siku ya Jumanne. Habari zilizochapishwa na tovuti ya Arabianbusiness zinasema kuwa nuskha hizo zilikuwa za shule moja katika mkoa wa Taif. Askari wa kuamrisha mema na kukataza maovu wa Saudi Arabia tayari wameanzisha uchunguzi kuhusiana na suala hilo na inasemekana kuwa idara ya masomo na malezi ya mkoa huo itasailiwa kuhusiana na tukio hilo la kusikitisha. 767256
captcha