IQNA

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa alaani uchomwaji moto Qur'ani Tukufu nchini Marekani

10:59 - April 06, 2011
Habari ID: 2101469
Ban Ki-moon Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa jana Jumanne alilaani uchomwaji moto Qur'ani Tukufu uliofanywa na kasisi mmoja wa Marekani katika jimbo la Florida.
Akilaani kitendo hicho cha dharau, Ban amesema kuwa hakuna dini yoyote duniani inayoruhusu kukosewa heshima matukufu ya dini nyinginezo. Katibu mkuu huyo alilaani kitendo hicho alipoonana na kuzungumza na wawakilishi wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu katika Umoja wa Mataifa ambao ni mabalozi wa Misri, Morocco, Pakistan, Iran na Tajikistan katika umoja huo. Baada ya mazungumzo hayo, Ban amesema kuwa kitendo hicho cha kukera cha Kasisi Terry Jones kitaamsha hasira za Waislamu katika pembe mbalimbali za dunia na kusema kuwa tayari kimeshasababisha wahanga katika nchi ya Afghanistan ambapo watu 12 wamepoteza maisha yao katika maandamano ya ghasia yaliyofanyika nchini humo hivi karibuni. 769720
captcha